MAWASILIANO

Phone. - +255 (717) 300 260 - +255 (787) 300 260

HABARI YA MUJINI

HABARI YA MUJINI
watu wa mpira

KERR AENDELEA KUSISITIZA KUWA YANGA NI TIMU YA KAWAIDA SANAAA


Na Nassor Amour, Zanzibar
Kocha Mkuu wa Simba, Dylan Kerr, ambaye juzi Jumatano alikiacha kikosi chake kikiendelea na mazoezi kisiwani Zanzibar na kwenda Uwanja wa Taifa jijini Dar kushuhudia robo fainali ya Kombe la Kagame, kati ya Yanga na Azam, amesema Yanga ni timu ya kawaida sana.


Kocha huyo amesema anashangaa viongozi wake kumueleza kila siku kuwa aifunge Yanga wakati yeye anaiona ya kawaida sana.
Akizungumza mjini hapa, Kerr alisema ameiona mechi hiyo na kusema si kwamba Yanga hawana wachezaji wazuri lakini Azam walifanya vizuri zaidi licha ya kwenda sare mpaka kufikia hatua ya matuta.

 “Kutokana na msisitizo huo, nimelazimika kufuatilia baadhi ya mechi za timu hiyo, nimeona mambo kadhaa lakini sioni la ziada katika timu hiyo nikiilinganisha na kikosi changu ambacho nasikia nitaletewa wachezaji wengine wa kimataifa kwa ajili ya kukiimarisha.

“Yanga waliocheza juzi ni wa kawaida sana na hawatishi,” alisema Kerr.


Hii ni mara ya pili kocha huyo wa Simba akitamkia neon hilo kwamba Yanga ni timu ya kawaida sana.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment