Mbwana
Samatta akivalishwa taji na mdogowake muda mfupi baada ya kuwasili
kwenye uwanja wa ndege wa Mwl. Julius Kambarage Nyerere leo asubuhi
Familia ya Mzee Ally Samatta leo ilikuwepo uwanja wa ndege wa
kimataifa wa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere kwa ajili ya kumpokea na
kumpongeza mtoto wao Mbwana Samatta kwa mafanio makubwa aliyoyapata
kwenye soka kwa kutwaa ubingwa wa Afrika pamoja na kuwa mfungaji bora wa
michuano hiyo kwa mwaka huu. Mbwana Samatta (kulia) akilakiwa na babayake mzazi mzee Ally Samatta
Mzee Ally Samatta ambaye alikuwa ameambatana na familia nzima
wakiwemo kaka na wadogo zake Mbwana Samatta amesema, hawajawahi kwenda
kumpokea Samatta uwanja wa ndege wakiwa kama familia lakini leo waliamua
kufanya kitu cha tofauti kwasababu wanahisi hakuna kitu kingine ambacho
wanaweza kukifanya kikamfurahisha zaidi ya kwenda uwanja wa ndege kama
familia na kumlaki mtoto wao. Samatta (katikati) akiwa pamoja na familia nzima iliyokwenda uwanja wa ndege kumpokea
Mara baada ya kutua uwanja wa ndege, Samatta alijikuta akishindwa
kujizuia kuonsesha furaha aliyokuwanayo baada ya kukutana na familia
yake nzima ikiwa inamsubiri uwanjani hapo kwa ajili ya kumpongeza kwa
mafanikio yake pamoja na kusalimiana nae.
Mdogowake Samatta akamvalisha taji kakayake kama ishara ya ushindi na pongezi kwa kile mbacho tayari amefanikiwa mpaka sas.
Mashabiki na wadau wa soka nao wakaungana na familia hiyo kumpongeza
Samatta ambaye alikuwa ameambata na Thomas Ulimwengu kabla ya
kuchukuliwa na viongozi wa TFF na kupelekwa sehemu maalumu ambako
watapumzika wakisubiri kuingia kambini kuungana na kikosi kizima cha
Stars.
This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
0 comments:
Post a Comment